Please note that Tapas no longer supports Internet Explorer.
We recommend upgrading to the latest Microsoft Edge, Google Chrome, or Firefox.
Home
Comics
Novels
Community
Mature
More
Help Discord Forums Newsfeed Contact Merch Shop
Publish
Home
Comics
Novels
Community
Mature
More
Help Discord Forums Newsfeed Contact Merch Shop
__anonymous__
__anonymous__
0
  • Publish
  • Ink shop
  • Redeem code
  • Settings
  • Log out

FATHER & DAUGHTER (Swahili)

BINTI DHIDI YA BABA

BINTI DHIDI YA BABA

Sep 29, 2022


UPANDE WA OFISI ZA JOY

Damian amemaliza kuongea na waandishi wa habari baada ya kuzindua toleo jipya la nguo.

Damian: Hey!! Madam yukowapi?

Mfanyakazi-Sekretali: Madam ameondoka amenambia nikutarifu anaenda kumfata Eva.

Damian: Oooh!! mbona hajanisubiri.

                 :Ngoja nami nimfate (akawaza)

Damian akatoka ofisini na kuelekea eneo alipopaki gari yake ( parking )  lakini kwa bahati nzuri kabla hajafika kwenye gari yake, gari ililipuka na kumrusha mbali kama mita 10 kutoka eneo ilipokuwa gari, alijeruhiwa kidogi na vipande vya moto vilivyoruka baada ya mlipuko wa bomu pia aliumia baada ya kutua vibaya aliporushwa na bomu. Waandishi wa habari waliokuwa maeneo hayo wakaripoti tukio hilo.

CHUO KIKUU (UDSM)

Eva akiwa anatoka chuo yeye pamoja na rafiki zake, akiwa anawasubiria wazazi wake wampitie.

Eva: Wooow!! leo nimefurahi sana, vazi letu kuchaguliwa kuwa namba moja.

Rafiki: Yaani! hii itabidi i-trend lazima niweke kwenye mitandao tupate maoni pia.

Lakini ghafla rafiki yake alishikwa na butwaa.

Rafiki: Mungu wangu Eva, Eva!! angalia hii habari…!!

Eva: Hii ni kampuni ya mama yangu, gari iliyolipuka ni gari ya baba yangu wa kambo.

Eva ikabidi achukua usafiri haraka awai kwenda eneo la tukio.

Eva: Chidy unaweza kuniazima pikipiki yako…?

Chidy: Leo imekuaje mtoto wakishua unaniomba pikipiki!!?

Eva: Ok poa niambie itagharimu shingapi?

Chidy: Hayo ndio maneno, nipe mkono.

Eva: Ok chukua hii 60.

Eva akachukua pikipiki akaondoka haraka kuwai eneo la tukio.

NYUMBANI KWA MADAM JOYCE.

Madam Joyce anapigiwa simu na mfanyakazi wa kampuni yake.

Joyce: Haloo!!

Mfanya: Haloo! madam njoo haraka ofisini kunatatizo limetokea, kunamripuko, gari ya boss Damian imeripuka.

Joyce: Eti Nini!!, Damian amepona!

Simu ikakata Joyce akangia mtandaoni kuangalia habari  akakuta mitandaon imeenea habari hiyo tu. Haraka haraka akaeleke eneo la tukio.

OFISI ZA JOY

Eva amefika katika ofisi za mama yake anakuta watu wamejaa Polisi na zimamoto wameshafika pia anamkuta baba yake wa kambo yupo pembeni na watu wa huduma ya kwanza.

Eva: Baba baba, uko salama baba yangu?

Damian: Ndio nipo salama Eva, nimejeruhiwa kidogo tu.

Eva: Vipi mama yeye yuko wapi? Je yupo salama?

Damian: Ndio mama yako alitangulia kukufata itakuwa umepishana nae.

Eva: Pole sana baba yangu... (akiwa analia)

Madam Joyce pia akafika eneo la tukio.

Joyce: Damian uko salama!?

Damian: Ndio niko salama Joyce.

Joyce: Shida nini!? gari ilikua na shida gani!

Damian: Mripuko wa bomu.

Joyce: Bomu!!?

Damian: Ndio wataramu wamesema hilo ni bomu la kutega na sio mlipuko wa mafuta.

Joyce: Nani sasa amefanya hivi?

Damian: Bado sijajua Joyce.

Eva: Mimi namfahamu..!! (Kwa hasira)

Eva akaondoka eneo lile akiwa na hasira akachukua pikipiki aliyokujanayo akawasha na kuondoka huku mama yake

Joyce: Evaaa subiri, unaenda wapi wewe, mwanangu nisubiri.. Acha kufanya hicho unachotaka kufanya. Evaaa!!

Madam Joyce na yeye pia akachukua gari yake na  kuanza kumfukuzia Eva, Damian pia akawasukuma madaktari akachukua usafiri.

Damian: Hey! unaweza kuendesha gari vizuri?

Dereva-Tax: Ndio mzee.

Damian: Ok shika hii hela wafukuzie wale.

Damian akaingia kwenye gari na kuwafukuzia. Eva alikua na hasira sana akafika katika ofisi za PROUD akashuka kwenye pikipiki kisha akaingia ndani ya geti mlinzi moja akataka kumzuia lakini mlinzi mwingine aliekua amekaa pembeni anakula (bonge) akamwimbia.

Mlinzi1: Hey! Hey! madam simama, fata utaratibu wa kuingia ndani.

Mlinzi (Bonge): Wewe huyo ni mtoto wa boss usirudie kumzuia, huyo ni boss wako.

Mlinzi1: Mmmhh!

Eva akaingia ndani ya ofisi akiwa na hasira baadhi ya wafanyakazi wanao mfahamu wanamsalimia lakini hawajibu wanabaki wanashangaa!! Eva akaingia kwenye lifti kuelekea kwenye ofisi ya baba yake. Akabonyeza rimoti impeleke ghorofa ya 43.

Wakati huo Madam Joyce na yeye pia anafika katika ofisi za PROUD mlinzi anataka kumzuia.

Mlinzi1: Hey! Hey! madam simama, fata utaratibu tafadhali?

Mlinzi (bonge): wewe huyo ni mke wa boss. Unamzuia boss wako asingie ofisini mara ya tatu utafukuzwa kazi.

Mlinzi1: Aaaahhhg!!

Miss pia akaingia ofisini akiwa anakimbia kumuwai Eva wafanyakazi wakabaki na mshangao. Madam Joyce akaingia kwenye lifti pia akabonyeza namba 43. Wakati huo Damian na yeye anafika katika ofisi za PROUD. Akashuka kwenye gari akaingia ndani lakini mlinzi hakumzuia.

Mlinzi1: Mmmh!!?

Mlinzi (bonge): Vipi wewe mbona hujamzuia huyoo!! anaingia bila kufata utaratibu.

Mlinzi1: Oooh! vipi huyo sio muhusika hapa, sio shemeji yake boss au mjomba au rafiki yake boss!?

Mlinzi(bonge): Mkamate wewe huyo mzuie. Huyo sio muhusika hapa.

Walinzi wakaanza kumkimbiza Damian lakini alikua amewacha mbali akawai kufika kwenye lifti. Kutokana na kuwa mgeni kwenye ofisi zile hakujua Mr Moses anapatikana ghorofa ya ngapi hivyo akabonye namba 40. Wafanyakazi wakabaki na mshangao wasijue nini kinaendelea!

Wlinzi1: Wewe simamaa.

UPANDE WA EVA

Eva anaingia katika ofisi ya baba yake anamkuta baba yake kasimama akiwa anangalia nnje upande wa kioo akiwa na mawazo sana. Eva anachomoa bastora kisha akanyosha kuelekea kwa baba yake (akamnyoshea).

Eva: Babaaaa..!!

Moses anageuka kwa mshtuko anashangaa kumona Eva amemnyoshea bastora huku akitokwa na machozi.

Mr Moses: Please!! Eva usifanye hivyo!!

*** ITAENDELEA ***  -  Jumatatu 3 October 2022

custom banner
petercharlz255
BOBOtheBEST-Comics

Creator

YALIYOMO KWENYE EPISODE YA MWISHO - IJAYO (EP 08)
...
Eva: Usinisogelee nijibu kwanini unataka kuwaua wazazi wangu!? (kwa hasira)
...

Eva: Baba wewe muongoo. (kwa uchungu)
....

Joyce: Evaaa hapanaaaa, Evaaaaa!!!
...

Eva: Mama nambie ukweli maana mi sielewi.!!

Joyce: Usijalaumu mwanangu sio baba yako wala wewe mwenye makosa lakini mimi ndie mwenye makosa.
...

Joyce: Mimi na baba yako tulipendana sana, na hatukujua kama siku moja tutakuja kuachana na kusbabisha...
...

Eva: Ugomvi ulisbabishwa na nini?

Mam: Kipindi kampuni yetu inakua watu...
...

Eva: Mama…!! Yule mwanamke ni nani? Na kwanini alikuja kuharibu ndoa yenu!?

Mam: Leo ndio nimegundua yule mwanamke ni nani.

Eva: Ni nani?
...
Mlinzi1: hey!! Simama hapo hapo, jisalimishe mwenyewe.

Mlinzi(bonge): Simama bana!! Mambo gani haya unatukimbiza kama watoto.

Damian: (akanyosha mikono juu) Saw ninajisalimisha, lakini nisikilizeni boss wenu itakua amepatwa na tatizo humu ndani maana na...
...

Eva: Mamaaaa….!!? hapana!
...

Lakini Eva hakumjibu chochote.

Damian: Eva nini kimetokea mwanangu!?
...
Damian: (Akawaza) Inawezekana Eva kaujua ukweli nini!! Mbona hanijibu!?
...

Eva: Ulisema kweli!! Unapo lenga kuwa makini, usipoteze shabaha. Nimefanya hivyo Damian.
...

Polisi: Mkuu, tumefanikiwa kumfahamu mtu alieweka Bomu kwenye gari ya Mr Damian.

Polisi (mkuu): OK!! chukua kikosi mara moja mkamkamate, pengine anaweza pia akawa muhusika wa...
...

Hakimu: kutokana na ushahidi tuliopata kwa muda mrefu sasa imengundulika kuwa Eva Moses...
...

Mwandishi: Asante sana Madam Eva !! Watu wanasema ume...
...

USIKOSE EPISODE IJAYO - Jumatatu 3 October 2022

#fatheranddaghter #bobothebestcomics #bobothebeststudios #petercharlz255

Comments (2)

See all
Edu sal
Edu sal

Top comment

Ila ngojaa tungojee

1

Add a comment

Recommendation for you

  • Secunda

    Recommendation

    Secunda

    Romance Fantasy 43.3k likes

  • Invisible Boy

    Recommendation

    Invisible Boy

    LGBTQ+ 11.4k likes

  • What Makes a Monster

    Recommendation

    What Makes a Monster

    BL 75.3k likes

  • Silence | book 1

    Recommendation

    Silence | book 1

    LGBTQ+ 27.2k likes

  • For the Light

    Recommendation

    For the Light

    GL 19.1k likes

  • Silence | book 2

    Recommendation

    Silence | book 2

    LGBTQ+ 32.3k likes

  • feeling lucky

    Feeling lucky

    Random series you may like

FATHER & DAUGHTER  (Swahili)
FATHER & DAUGHTER (Swahili)

1.6k views5 subscribers

Mr Moses katika maisha yake yote licha ya kuwa na utajiri mkubwa lakini kuna kitu kimoja anakipenda kuliko vitu vyote. Mr Moses anampenda binti yake (Eva) kuliko mtu yoyote kuliko kitu chochote kwenye hii dunia yenye mabilioni ya watu na vitu. Lakini anajikuta anaingia kwenye wakati mgumu baada ya binti yake Eva Moses anapobadilikaka na kuwa adui yake mkubwa...
Subscribe

8 episodes

BINTI DHIDI YA BABA

BINTI DHIDI YA BABA

143 views 2 likes 2 comments


Style
More
Like
List
Comment

Prev
Next

Full
Exit
2
2
Prev
Next