Please note that Tapas no longer supports Internet Explorer.
We recommend upgrading to the latest Microsoft Edge, Google Chrome, or Firefox.
Home
Comics
Novels
Community
Mature
More
Help Discord Forums Newsfeed Contact Merch Shop
Publish
Home
Comics
Novels
Community
Mature
More
Help Discord Forums Newsfeed Contact Merch Shop
__anonymous__
__anonymous__
0
  • Publish
  • Ink shop
  • Redeem code
  • Settings
  • Log out

FATHER & DAUGHTER (Swahili)

BABA BORA

BABA BORA

Sep 24, 2022

Mwandishi wa kitabu: Peter Charlz
Mchoraji: Peter Charlz
Instagram / Twitter / Facebook: @petercharlz255
Email: petercharlz255@gmail.com

Shukrani za dhati kwa kila alieshiriki kuandaa kitabu hiki.
Mhakiki : Augustino Peter
Instagram : babadenze

BOBOtheBEST Studios
Instagram: bobothebeststudios & bobothebestcomics
Facebook: bobothebestproduction
Email: bobothebestproduction@gmail.com

LUGHA
Lugha iliyotumika ni kiswahili ambacho kinatumika katika mazingira yetu ya kilasiku. Hatujatumia ufasaha wa lugha ya kiswahili lakini tumeangalia mazungumzo ya kawaida yanayofanyika mitaani, kwenye familia n.k. Baadhi ya misamiati imetumika lugha ya kingereza ili kuweka uhalisia wa mazungumzo ya kilasiku katika jamii zetu, hasa katika hiki kizazi kipya.


BOBOtheBEST Studios
Presents



Karibu jiji la Dar-es-salaam katika nyumba moja ya kifahari ya tajiri mmoja mwanamitindo Bwana Moses (Mr Moses). Mr Moses amekuwa tajiri mkubwa kutokana na kampuni yake ya mavazi inayoitwa Proud (Fahari) inayofanya kazi zake nchini na nchi jirani. Amejipatia umaarufu mkubwa nchi nzima kutokana na bidhaa zake nzuri na zenye ubora wa hali ya juu. Na leo katika nyumba yake ametembelewa na wandishi wa habari ambao wamekuja kufanya mahojiano na binti yake Mr Moses ambae hivi karibuni anatarajia kuzindua toleo jipya la nguo. Binti huyu anaitwa Eva Moses, mtoto wa tajiri mkubwa mwanamitindo Mr Moses…

Mtangazaji (ke): Wewe ni binti mdogo sana umesema una-umri wa miaka 17 tu, unawezaje ku-design (kubuni) mavazi mazuri hivi kama mtu ambae umri wake ni mkubwa?

Eva (binti): Woow!! Labda kitu ambacho watu wengi hawajui kuwa, hii ni talent kutoka kwa wazazi wangu. Wazazi wangu wote wawili ni wanamitindo na pia wanaendesha kampuni kubwa za mavazi. So, naweza sema hii nimezaliwa nayo lakini kwa kuongezea tu, hii kitu ndio nayosomea yaani nasomea maswala ya mavazi.

Mtangazaji (ke): Unasomea ubunifu wa mavazi?

Eva: Yeah!! Nasomea fashion kama modeling, designer, marketing n.k. katika maswala ya mavazi.

Mtangazaji (ke): Oooh!! Hongera sana!

Eva: Asante!! Asante sana.

Mtangazaji (ke): Ok! Swali ambalo napenda kumalizia nataka kujua au mtazamaji anayetaka kujua, Eva anapenda nini kuliko kitu chochote katika maisha yake?

Eva: Kitu nachokipenda kuliko chochote!?

Mtangazaji (ke): Ndio.

Eva: Wooow!! Kitu amabacho napenda kuliko kitu chochote katika maisha yangu ni baba yangu. Baba yangu Mr Moses nampenda sana, sana yani siwezi hata kuelezea ila kwangu yeye ndio namba moja.

Wakati mahojiano yanaendelea Mr Moses alikua pembeni kidogo akimuangalia binti yake akifanya mahojiano, mwandishi mmoja alimfata Mr Moses.

Mwandishi (me): Hongera Mr Moses kwa mambo makubwa unayoyafanya.

Mr Moses (baba): Asante sana!!, Asante kwa mchango wenu pia.

Mwandishi (me): Vipi muingize binti yako sasa katika kampuni yako, maana anafanya mambo makubwa pia.

Mr Moses : Yeah!! ni Kweli, lakini nataka kwanza amalize kusoma na umri uende kidogo yaani walau akiwa hata na miaka 19 au 20 hivi.

Mwandishi (me): Ooohh! Kweli akili ikue pia.

Wakati wakiendelea na mazungumzo Eva alikua amemaliza kufanya interview (mahojiano), anaenda alipo baba yake.

Mwandishi (me): Oohoo!! naona wamemaliza, ok sawa Mr Moses tutaonana siku nyingine.

Mr Moses : Sawa asante sana aisee, karibuni tena. (wakaagana)

Eva: Baba…!! (kwa furaha)

Mr Moses : Eva binti yangu, hongera kwa bonge la interview. Umefanya interview ya dunia.

Eva: ha ha ha ha ha..! Acha utani baba.

Basi siku hiyo ilikua siku ya furaha kwa familia hiyo ambayo ina-jumla ya watu 27 na 25 kati yao ni wafanyakazi ukimtoa Mr Moses na Eva. Siku iliyofuata asubuhi na mapema Mr Moses anaamka anaingia bafuni anapiga mswaki kisha anoga na ananza kujiandaa, inaonekana kunasehemu anataka kwenda. Baada ya muda anamaliza kujiandaa anatoka chumbani kwake.

Mr Moses : Heloo!! Eva, Eva umejiandaa tuondoke?

Eva: Ndio baba, Madam Sarrah anamalizia kuniandaa hapa.

(Madam Sarrah/Bi Sarrah ni kijakazi wa Eva)

Mr Moses : Ooohhoo!! Nimegundua kitu, naona unataka upendeze mpaka umshinde mwenye sherehe.

Bi Sarrah: Nimemvalisha nguo hiyo kwasababu ni rangi anayoipenda sana mama yake.

Mr Moses : Yeah!! Mama yake akiona atafurahi, atafurahi hasa akiona amevaa mtoto wake.

Eva: Wooow!! leo tunaenda kumuona mama, nataka nimuone  mama harisi sio picha tena. Na nikimaliza muda wa likizo nitamwambia mama turudi wote huku.

Mr Moses alishtuka kidogo baada ya kusikia hivyo lakini akapotezea.

Mr. Moses: Yeah! vizuri.

                    : Aya sawa, sasa uko tayari twende maana tunachelewa.

                    : Bi Sarrah umemuwekea vizuri mizigo yake?

Bi Sarrah: Ndio tayari nimeweka vitu vyote alivyonielekeza.

Mr Moses : Eva umekumbuka kuchukua vitabu?

Eva: Ndio baba, nimekumbuka.

Mr Moses : Vizuri usiache kusoma unatakiwa ufanye vyote ulivyokuwa unafanya huku. Sawa?

Eva: Sawa baba.

Baada ya kuchukua mizigo yao Mr Moses na Eva walingia kwenye gari safari ikaanza, wakiwa ndani ya gari mazungumzo yaliendelea kati ya baba na binti.

Eva: Baba leo ni siku ya kuzaliwa mama?

Mr Moses: Hapana mwanangu..!! Sherehe tuanyoenda ni harusi.

Eva: Mmmh!! OK.

Baada ya safari ya masaa mawili (2) njiani hatimaye safari yao imefika eneo husika, eneo la sherehe. Ni katika jumba jingine kubwa la kifahari na inaonekana kuna watu wengi sana, sherehe imefana kweli kweli. Mr Moses na binti yake walipokelewa.

Mlinzi: Karibu mheshimiwa!! samahani nione Kadi zenu.

Mr Moses: Kadi hii hapa, tunatumia kadi moja ya double.

Mlinzi: Ok VVIP unapita mlango huu utakuta meza yenye jina lako.

Mr Moses: Sawa boss asante!! Eva tangulia twende mwanangu kipenzi.

Eva: Wooow!! puzuri pamependeza.

Mr Moses: Pamendeza sana kama ulivyo pendeza leo mrembo wangu.

Walifika katika meza za VVIP kisha wakakaa kwenye meza yao huku sherehe ikaendelea, Sherehe husika ilikua ni harusi kubwa ya kifahari  inaendelea pale mbele, huku bwana harusi pamoja na bi harusi wakisalimiana na wageni walikwa. Ilikuwa ni siku nzuri ya furaha.

Bwana hurusi (Damian): Bado sijamuona Mr Moses?

Bi harusi (Joyce): Mimi nachohitaji kwa sasa ni kumuona mtoto wangu tu. Ni miaka mingi sasa nipo mbali nae.

Damian: Vipi hujamkumbuka mumeo ha ha ha ha !? (kejeri)

Joyce: Sipendi kuliongelea hilo hapa, ukizingatia leo ni siku gani kwetu.

Katika meza aliyokaa Mr Moses na binti yake mazungumzo yanaendelea taratibu huku wakipata vinywaji.

Eva: Oooph!! watu ni wengi nimejaribu kuangalia labda naweza kubahatisha nimuone mama lakini sijapata chochote.

Mr Moses: Usijari Eva muda ukifika utamuona.

Eva: Oooh woow!! Baba nimemuona mama!! yulee.( kwa furaha)

Eva alinuka kwenye kiti alichokuwa amekaa kisha akanza kumkimbilia mama yake lakini kabla hajamfikia mama yake alisimama ghafla!!  Amepigwa butwaa baada ya kuona mama yake amemshika mkono mwanaume mwingine, Lakini…

Mr Moses: Oooh! Usiogope twende kwa mama.

Eva: Mama amemshika mkono huyo! huyo ni nani?

Mr Moses : Ndio, ndio nimekumbia leo tunakuja kwenye sherehe ya mama yako sawa, usiogope twende.

Wakasogea karibu.

Damian: Aaahhaa! Karibu Mr Moses… Naona upo na binti yako.

Mr Moses: Asante sana Mr Damian mambo vipi!?

Damian: Tuko poa kama unavyona watu wanafurahi naamini hakuna aliejutia au sio Mr Moses.

Mr Moses: Ni kweli, ni kweli kabisa Damian, sherehe ni nzuri kuanzia mazingira, chakula, muziki mpaka wahusika nyinyi wenyewe mmependeza...  Mambo vip Joyce?

Joyce: Mi niko poa, karibuni sana… Woow!! Eva binti yangu hujambo, niliku-miss sana mumy.

Eva: Mama huyu nani?

Joyce: Huyu? (Kwa wasiwasi)

Eva: Ndio.

Joyce: Aaaahh mmh!!

Mr Moses: Eva huyu ni baba yako.

Eva: Baba yangu ni wewe tu.

Mr Moses: Namanisha huyu ni baba yako mlezi na mimi ni baba yako mzazi. yaani huyu ni baba yako mwingine, baba wa kambo.

Eva: Hapana haiwezekani.

Mr Moses: Kwanini, ni baba yako, anakupenda… anakupenda kama anavyokupenda mama yako... Ni baba mzuri, sawa usimuogope. (akibembeleza)

Eva: Kwaiyo likizo yote nitakuwa nakaa na mama na huyu baba mwingine.?

Mr Moses: Ndio… Huyo sasa ni baba yako kwasababu leo amefunga ndoa na mama yako.

Eva: Inamaana leo ni harusi ya mama...!! Mbona sielewi... Yaani!! namanisha wewe baba harusi yako lini? (kwa mshangao)

Mr Moses: Harusi yangu!?, haipo na wala hautakuja kuiona.

Eva: kwanini baba!! Wakati mama yeye ameolewa?

Mr Moses: kwasababu harusi yangu ilikuwa kabla ya wewe kuzaliwa.

Eva: Unamanisha harusi yako na mama?

Mr Moses: Ndio mwanangu.

Eva: Sasa mbona wewe baba haukai na mama mwingine?

Mr Moses: Sina uhitaji kwasababu.., kwasababu maishani mwangu nimepata kilakitu.

Eva: kilakitu!!? Nini, kwasababu wewe ni tajiri?

Mr Moses: Hapana, kilakitu ambae ni wewe. Wewe ndio kila kitu kwangu.

Eva alifarijika kwa maneno hayo mpaka ikampelekea akamkumbatia baba yake na kujibu.

Eva: Wewe ndio kilakitu kwangu baba, nakupenda kuliko kitu chochote na sitaki uwe na mama mwingine lakini mama ni mbaya kwanini hakukaa na wewe baba.

Mr Moses: Usiseme hivyo mimi ndio niliemkosea mama, sio yeye. (kumfariji)

Eva: Unasema kweli baba, wewe ndio ulimkosea?

Mr Moses: Ndio mwanangu, Lakini unajua nini kilitokea baada ya kumkosea?

Eva: Hapana sijui, kilitokea nini !?

Mr Moses: Nilimuomba msamaha mama yako na akanisamehe. Alinisamehe kwasababu sisi ni binadamu na sio mara zote tunafanya kilicho sahihi, kuna muda tunakosea ndio maana inatubidi tusamehe kabla haijafika kipindi ambacho na sisi tunahitaji msamaha tunapokosea. Kwahiyo wewe pia unatakiwa utusamehe mimi na mama yako tulishindwa kukaa pamoja.

Joyce: Inatosha sasa Moses, nafikiri mtoto amekuelewa na atafanya kama ulivyomuelekeza.

Mr Moses: Ok sawa!! Eva kwa muda wa likizo yote hii, utabaki kwa mama pamoja baba hapa arafu baada ya likizo nitakuijia sawa.

Eva: Usichelewe kunijia maana nitakuwa nimekukumbuka sana.(kwa utani)

Mr Moses: Usijali nitamuambia dereva anikumbushe nisije sahau (utani). Aya Eva, Joyce na Damian mi niwaache sasa, lakini nilikua na hii zawadi kwa Joyce. 

Joyce: Asante Mr Moses kwa zawadi yako.

Mr Moses akam-kiss Eva kisha akaingia kwenye gari akaondoka. Eva akamuangalia mama yake pamoja baba yake wa kambo, akawambia.

Eva: Nawapenda mama na baba yangu, nitawapenda kama nilivyoambiwa niwapende na baba yangu.

Damian: (Akawaza) inaonekana anampenda, anamsikiliza na kumuamini sana baba yake.

               (kisha akamuuliza:)...

*** ITAENDELEA ***


Soma hapo chini kwenye description kujua yaliyomo kwenye episode ijayo. 

custom banner
petercharlz255
BOBOtheBEST-Comics

Creator

YALIYOMO KWENYE EPISODE IJAYO (EP 02)
...
Damian: (Akawaza) Inaonekana anampenda, anamsikiliza na...
(kisha akamuuliza) Unakumbuka baba amekuambia nini kuhusu mimi..?

Eva: ...!!

Damian: Usiogope mwanangu baba yako hajakudanganya, unachotakiwa ni...
...

Joyce: Wooow!! vizuri mtoto wangu mzuri, nafurahi kusikia mwanangu umepapenda nyumbani.

Eva: Oohh!! lakini nimeshindwa kufanya kimoja...

Joyce: Kipi hicho mwanangu ?

...
Mr Moses: Woow! Nilikuambia utanisahau tu (utani)

Eva: Siwezi kukusahau baba yangu, iyo siku haipo.
...

Damian: Mmhh!! kati ya baba na mama yako unampenda nani zaidi?

Eva: Nampenda zaidi baba.
...
Damian: Ooohh!!Mungu msamehe binti huyu, anahukumu bila kujua chochote.(kwa sauti ya chini)

Eva: Kwanini Mungu anisamehe?

Damian: Nasikitika hujui nini sababu ya mama...
...
Eva: Sawa nenda, niache kwanza. (kwa hasira)

Damian: Sawa Eva najua nimekumiza lakini...

USIKOSE EPISODE IJAYO.

#fatheranddaghter #bobothebestcomics #bobothebeststudios #petercharlz255 #Seasonone

Comments (7)

See all
Edu sal
Edu sal

Top comment

BtB imekaa poa dingiii acha tungojee na mwendelezo upoje BtB one love Guy's....✊️

2

Add a comment

Recommendation for you

  • Secunda

    Recommendation

    Secunda

    Romance Fantasy 43.3k likes

  • What Makes a Monster

    Recommendation

    What Makes a Monster

    BL 75.3k likes

  • Invisible Boy

    Recommendation

    Invisible Boy

    LGBTQ+ 11.4k likes

  • For the Light

    Recommendation

    For the Light

    GL 19.1k likes

  • Silence | book 2

    Recommendation

    Silence | book 2

    LGBTQ+ 32.3k likes

  • Blood Moon

    Recommendation

    Blood Moon

    BL 47.6k likes

  • feeling lucky

    Feeling lucky

    Random series you may like

FATHER & DAUGHTER  (Swahili)
FATHER & DAUGHTER (Swahili)

1.6k views5 subscribers

Mr Moses katika maisha yake yote licha ya kuwa na utajiri mkubwa lakini kuna kitu kimoja anakipenda kuliko vitu vyote. Mr Moses anampenda binti yake (Eva) kuliko mtu yoyote kuliko kitu chochote kwenye hii dunia yenye mabilioni ya watu na vitu. Lakini anajikuta anaingia kwenye wakati mgumu baada ya binti yake Eva Moses anapobadilikaka na kuwa adui yake mkubwa...
Subscribe

8 episodes

BABA BORA

BABA BORA

548 views 5 likes 7 comments


Style
More
Like
List
Comment

Prev
Next

Full
Exit
5
7
Prev
Next